TEGETA SDA

TEGETA SDA

SEMINA KUHUSU KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO NA MFUMO WAKE[1] KANISA LA TEGETA SDA TAREHE 6 APR 2013





1.      UTANGULIZI

·            Agizo la injili la Mwokozi wetu Yesu Kristo la kupeleka injili ulimwenguni kote ni kazi yenye utisho (Math 28:19, 20). Madhehebu yote yanakubali kwa kiasi fulani wajibu huu. Lakini Waadventista Wasabato wanasimama peke yao katika kujisikia kuwajibika katika kupeleka ujumbe wa malaika wa tatu “kwa kila taifa, kabila, lugha na jamaa (Uf. 14:6).

·            Hivyo, mfumo wa kanisa ni wa lazima katika kutekeleza agizo hilo.

·            Kanisa mahalia lolote lile linalolenga katika shughuli mahalia tu limepoteza njozi ya pekee ya kanisa la waadventista Wasabato kiulimwengu (Mwongozo wa Wazee, 2007 Uk. 22; Kazi ya sadaka za kila robo – Angalia “Lesson ya watu wazima, Robo II, 2013).

·            Waadventista Wasabato wanaamini kwamba kazi haitamalizika popote mpaka imalizike kote.

·            Mtazamo wa kanisa kiulimwengu huleta changamoto kubwa ya kimfumo, hivyo:

Ø   Hainabudi mfumo wa kanisa ieleweke kwa kila muumini kanisani.

Ø   Mfumo lazima uwe wa ufanisi.

Ø   Kazi ni ya kiulimwengu mzima hivyo lazima yawepo mamlaka ya kutosha yaliyobainishwa kwa ngazi za utawala nje ya kanisa mahalia ili kuwe na uhakika wa mgawanyo wa ulinganifu wa watendakazi na pesa;

Ø   Kazi ni ya mataifa mengi na tamaduni nyingi hivyo mfumo haunabudi kuwa unaoweza kubadilika kirahisi kupokea mazingira mapya  (flexible) (Uf 14:6).

2.      HISTORIA YA MWANZO WA WAADVENTISTA WA SABATO

·         Historia ya mwanzo wa Waadventista inaanzia kwa mhubiri mashuhuri William Miller (1782).

·         Miller alikuwa Mkristo Mbaptisti, lakini hakuridhika na kanisa lake, kwa kutojibu maswali yake mengi yaliyokuwa yanamsumbua.

·         Mwaka 1816 (akiwa na miaka 34 tu) alianza kusoma na kuchunguza Biblia kwa dhati.

·         Katika usomaji huo alitafsiri Dan 8:14 na kufikia uamuzi kuwa Yesu angerudi tarehe 22 Oktoba 1844.

·         Miller alianza kuhubiri kwa nguvu juu ya kurudi kwa Yesu mara ya pili 14 Agosti 1831. Aliendelea kuhubiri kwa miaka 13 (www.sdaisrael.org – Our Identity).

Ø   Alitoa mahubiri 4,000 katika miji 500.

Ø   Zaidi ya wachungaji (clergy) 200 walimwamini.

Ø   Watu wapatao 100,000 waliamua kumfuata na waliitwa “Millerites”.

·         Siku hiyo ilipofika na Yesu hakuja ilikuwa ni siku ya huzuni kubwa (“Great Disappointment.”)

·         Wale waliosalia baada ya kukatishwa tamaa kikuu waligawanyika katika makundi mawili:

Ø   Wengine waliamini kuwa tukio la kurudi kwa Yesu lilikuwa sahihi ila tarehe ilikosewa, hivyo wakaanza kupanga tarehe zingine.

Ø   Kundi la pili walielewa kuwa Masihi angekuja haraka, kwamba wakati walitafsiri tukio vibaya, lakini tarehe ilikuwa sahihi. Walikataa kuweka tarehe nyingine mpya, na kugeukia Neno la Mungu, waliendelea kuchunguza ukweli wa Biblia kwa bidii. Waadventista Wasabato wametokana na kundi hili la pili.

·         Kadiri walivyoendelea kutafuta ukweli wa Biblia waligundua (rediscovered) ukweli wa sabato.

·         Wakati huo huo, Hiram Edson, mkulima mmoja (local farmer) huko Marekani, katika kujifunza Biblia alikuja kuelewa wapi William Miller alikosea katika kutafsiri patakatifu. Aligundua kuwa kulingana na Biblia, patakatifu pa duniani ilikuwa mfano tu wa patakatifu pa mbinguni (Kut. 25:9).

·         Maendeleo baada ya siku ya huzuni kubwa “Great Disappointment”:
1844-1863:
Ø   Joseph Bates na James White na Ellen White walisafiri kote katika New England wakiendesha madarasa ya Biblia, kuunda vikundi vya maombi, na kujenga umoja wa Mafundisho Makuu. Mama White alichangia kiasi kikubwa katika kazi hii.

Ø   Matokeo ya kazi yao ilizaa pamoja na mambo mengine: Utunzaji wa Sabato; Utunzaji wa miili yetu; na Kuishi kiafya na Imani katika kupeleka Injili.

1863 na kuendelea:
Ø   Mwaka 1863 Kanisa la Waadventista Wasabato liliundwa rasmi likiwa na waumini 3,500.

Ø   Makao Makuu ya Kanisa yalikuwa Battle Creek, Michigan Marekani (sasa yako Silver Spring Maryland, Marekani).

Ø   Mwaka 1900 waumini walimuwa 75,000; 1955 waumini zaidi ya waumini 1,000,000. Leo kanisa lina waumini wapatao milioni 20 duniani kote.


·         Mwaka huu, 2013 Kanisa la Waadventista Wasabato linatimiza miaka 150 tangu lianzishwe rasmi mwaka 1863 huko Marekani.

·         Sherehe za miaka 150 zitafanyika katika makanisa yote kote duniani. Mipango ya namna  makanisa yatakavyofanya sherehe hizo imeachwa kwa makanisa husika yenyewe au katika mitaa  yao, katika Konferensi au katika Union husika. Mambo muhimu yanayotiliwa mkazo katika sherehe hizo ni:

Ø   Kujikita katika Mafundisho Makuu  ya Imani

Ø   Uinjilist (Evangelism).

Ø   Utunzaji  (Nurturing & Retention).

Ø   Kujumuika kama  Familia ya Mungu (Fellowship)

3.      AINA YA MFUMO NA UTAWALA WA KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO

·         Kuna aina 4 za utawala wa kanisa
Na.
Aina ya Utawala
Mfumo wa Utawala
Mfano wa Kanisa




1.
Utawala wa Kipapa
Ambapo Papa ana mamlaka ya juu kabisa

Katoliki
2.
Utawala wa Kiaskofu
Mamlaka ya mwisho yapo kwa maaskofu wa kanisa

Lutheran & Anglican
3.
Utawala wa Kujitegemea
Mamlaka kamili ndani ya milki ya kanisa yapo kwenye kusanyiko mahalia

Makanisa ya Kipendekosti
4.
Utawala wa Kiuwakilishi
Mamlaka yapo kwa washiriki wa kanisa, lakini wajibu wa kupanga na kuratibu umeanishwa kwa ngazi nyingine.

Waadventista Wasabato

·         Kanisa la Waadventista Wasabato hufuata mfumo wa kiuwakilishi (ambapo kura ya wengi) katika utawala wake.

·         Si lazima watu wote wapige kura, maamuzi yanafanyika kwa wingi wa idadi ya watu waliopiga kura

·         Kazi ya kila ngazi ya Kanisa la Waadventista Wasabato hutathminiwa katika kila Sesheni (sessions) za kimihula (Kanisa Mahalia kila mwaka, Konferensi/Union/GC kila baada ya miaka mitano).

·         Katika Sesheni hizi taarifa zinatolewa, viongozi wanawajibishwa na uongozi mpya unachaguliwa.

·         Wajumbe wa sesheni hizi wanachaguliwa hasa na ngazi iliyo chini ya ile inayotathminiwa. Kwa mfano, kabla ya sesheni ya Konferensi mahalia kila kanisa wanachagua wajumbe kutoka katika waumini wake kuliwakilisha katika sesheni.

·         Awali wakati kanisa lilipoanza hapakuwepo na mfumo wo wote. Lakini kadri waumini na shughuli za kanisa zilipoendelea kuongezeka kukawa na haja ya kuwa na mfumo wa kanisa kwa sababu kuu zifuatazo:

Ø   Ili kuhifadhi na kumiliki mali za kanisa.

Ø   Ili kutambulisha yupi ni mchungaji wa kanisa letu wetu na yupi siye.

Ø   Ili kulipa wachungaji.

4.      MADARAJA YA MFUMO WA UTAWALA WA KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO


Mfumo wa Kawaida (Standard Design)

Mfumo Mbadala (Alternative Design)
1.
Kanisa Mahalia (Local Church)
1.
Kanisa Mahalia (Local Chrch)
2.
Konferensi Misheni  (Conf. Mission)
2.
Union of Churches
3.
Union Conference/Mission
3.
Division
4.
Division
4.
General Conference
5.
General Conference



5.      USHIRIKA (MEMBERSHIP)
Kanisa Mahalia
Watu
Konferensi Mahalia
Makanisa
Union
Ma-Konferensi
General Conference
Unions Conferences/Mission

1)         Ushirika Unapatikanaji

a.      Mtu hawezi kuwa mshiriki kwa mwenyewe, lazima kundi moja la watu wakufanye kuwa mshiriki. Ushirika ni haki/dhamana unayopewa na kanisa siyo mali yako. Unaweza kupewa na unaweza kunyang’anywa.

b.      Mtu hawezi kujibatiza mwenyewe, lazima ubatizwe na kundi Fulani ya watu.

c.       Ushirika kwa kanisa ni kwa njia moja tu kwa KURA.


2)         Mamlaka/Madaraka

a.       Katika Kanisa la Waadventista Wasabato mamlaka ya mwisho haikuachwa juu ya KUNDI (group) moja tu la waumini wala kwa MTU MMOJA au  KIKUNDI KIMOJA pekee yake.

b.      Mamlaka ya KUNDI la watu daima yako juu kuliko mamlaka ya mtu mmoja.

c.       MAMLAKA YA MWISHO (FINAL authority) haikuwekwa katika SEHEMU MOJA TU. Kila ngazi ya mamlaka ina baadhi tu ya madaraka.
Na.
Daraja la Utawala
Majukumu




1.
Kanisa Mahalia

-      Haina mamlaka yote bali baadhi tu.

-      Ina mamlaka ya mwisho tu juu ya ushirika wa mtu: nani awe mshiriki na nani asiwe mshiriki (ndiyo MAMLAKA YA MWISHO peke yake iliyonayo).

2.
Konferensi/Fildi/Misheni

-      Konferensi haina mamlaka yote bali baadhi tu.

-      Ina mamlaka ya mwisho tu juu ya Kupanga na kuondoa makanisa

3.
Union
-          Union inayojitegemea [union conference]
-          Union Misheni [union tegemezi], n.k.

-      Union haina mamlaka yote bali baadhi tu.

-      Ina mamlaka ya mwisho tu juu ya Kupanga na kuondoa ma-konferensi
4.
Halmashauri Kuu [general conference]

-      GC haina mamlaka yote bali baadhi tu.

-      Ina mamlaka ya MWISHO juu ya Misingi ya Imani na Kanuni za Kanisa




3)         Mamlaka ya kila ngazi na Athari (Impact) zake

·         Maamuzi yo yote magumu ya Kanisa mahalia yataadhiri àmoja kwa moja washiriki (watu) wa kanisa hilo tu. Mathalan, kufutwa ushirika n.k.

·         Maamuzi magumu ya Konferensi yataathiri àutendaji wa kanisa mahalia moja kwa moja. Hatua hiyo hatimaye yataathiri àwashiriki pia. Mathalan – kupewa karipio au kufutwa kwa kanisa.

·         Maamuzi magumu ya Union yataathiri àKonferensi mahalia na kwenda chini kwa àmakanisa yake na kwenda chini zaidi kwa àwashiriki wake. Mathalan kufutwa kwa Konferensi.

·         Maamuzi magumu ya GC yataathiri moja kwa moja àUnion husika na kwenda chini kwa àMa-konferensi na chini zaidi kwa àmakanisa ya konferensi hiyo na mwisho kabisa kwa àwashiriki. Kwa mfano kufutwa kwa Union.

Hivyo basi, mfumo wa kanisa la Waadventista Wasabato hatimaye hugusa kila mshiriki kwa hatua za maamuzi magumu.

6.      TAKWIMU ZA GC KUFIKIA JULAI 2012

a.    Total Members                            -        >17 million
b.    Local churches                            -        71,000
c.    Companies                                -        65,000
d.    Local Conferences                      -        321
e.    Local Mission                             -        264
f.     Union Conferences                     -        51
g.    Conference Mission                     -        55
h.    Union of Churches                      -        13?????
i.     Division                                     -        13
j.     GC                                            -        1
k.      Countries with SDA presence       -        209


IMETAYARISHWA NA:

Damba Omara
Mzee wa Kanisa


VIANZO REJEA: Kanuni za Kanisa Toleo la 17; Mwongozo wa Wazee – Kanisa na Mfumo Wake uk. 12-24; Semina ya Wachungaji na Wazee wa Kanisa, Morogoro, 24-27 Jani 2013; na www.sdaisrael.org – Our Identity).

No comments

Powered by Blogger.