TEGETA SDA

TEGETA SDA

MATANGAZO YA KANISA 20/04/2013



1. Tunamshukuru sana Mungu kwa kutulinda kwa wiki nzima hadi Sabato ya leo. Tunawakaribisha wageni kwa wenyeji katika Ibada ya leo.

2.  Sabato maalum ya wageni ilifanyika 13/04/2013, washiriki tunawashukuru kwa kuchangia gharama na kushiriki kualika wageni kwa ajili ya sabato hii muhimu. Mungu awabariki sana, tuendeleze moyo huu..

3. Mahubiri  katika Miji Mikuu yameshaanza Dodoma tarehe 13 – 28/04/2013. Tunashukuru kwa michango yenu tuendelee kuyaombea mahubiri haya.

4. Semina ya Kulea na Kutunza Washiriki ilifanyika kanisani Ilala tarehe 13-14/04/2013. Baraza la kanisa lilihudhuria. Tunawashukuru waliojitahidi kuhudhuria pia tunawatia moyo wengine kujenga tabia ya kuhudhuria semina muhimu kama hizi.

5. Kamati ya Majengo Mtaa itakutana Tegeta kanisani siku ya sabato leo (20/04/2013) saa 11 jioni. Wajumbe wote mnaombwa kuhudhuria bila kukosa.

6. Makambi ya mtaa yanaanza 21-27/07/2013; tutoe michango yetu (50,000/) kwa njia ya bahasha, muda unaisha.

7. Sensa ya washiriki ili kubainisha washiriki waliopo na wasiokuwepo itafanyika sabato ijayo 27/04/2013. Washiriki pitieni majina ubaoni, kwa ajili ya kuyatambua na kutoa taarifa kwa Karani/Kamati ya Baraza ya Sensa.

8. Sabato maalum kuchangia ujenzi wa nyumba ya mchungaji itafanyika tarehe 04/05/2013 kanisani Tegeta. Mnenaji mkuu anategemewa kuwa Pr. Toto Bwire Kusaga kutoka ETC. Goli letu ni kukusanya fedha si chini ya Milioni Ishirini (Tshs 20,000,000/=). Tunahimiza kila kanisa lijiandae vyema kwa tukio hilo muhimu.

9. Sadaka maalum ya kusaidia uanzishwaji wa Runinga (TV) ya Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania, Inaendelea kukusanywa tunahimizwa kila mtu achangie angalau Sh. 10,000/- goli la kanisa letu ni Sh. 3,300,000/-,bado hatujalifikia. Runinga itazinduliwa Juni, 2013.

10. Kesho (21/04/2013) tutakuwa na baraza la kanisa, wakuu wa idara andaeni mipango na taarifa za kazi, pia kamati mbalimbali malizieni kazi zenu na kuziwasilisha.

11. Baraza la Mtaa maalum litakaa tarehe 28/04/2013 kanisani Tegeta saa 3 asubuhi hadi saa 7 kamili mchana. Kikao hiki ni kwa ajili ya Mchungaji, Wazee wa Kanisa na Makarani wa Kanisa. Tafadhali zingatieni.

12. Katika ubao wa matangazo, kuna mapendekezo ya:

o    MAPENDEKEZO YA BAJETI YA KANISA, 2013
o    MAPENDEKEZO YA KALENDA YA MATUKIO YA KANISA, 2013

13. Konferensi yetu – ETC imetenga sabato ya tarehe 20/04/2013 kuwa Siku Kuu ya promosheni ya kununua na kusambaza kitabu cha “Tumaini Kuu” awamu ya pili. Kila kanisa linahimizwa kufanya hivyo. Lengo ni kununua vitabu 610,000 na zaidi katika awamu hii.

14. Juma hili, kuanzai kesho, tutakuwa na juma la uamsho na Roho ya Unabii, tuhudhurie kila siku saa 11:00, masomo maalumu yamewasili, juma hili litaendeshwa na Mzee Eraga Mjuli.

15. Maombi ya Jumatano asubuhi yanaendelea saa 11:00 asubuhi, na jioni tunawaalika wote kushiriki.

16. Ndoa: (Mara ya Tatu)

-          Mussa Wilson Sango (Tegeta SDA) na Agape Denis Bhoke (Kijenge SDA-Arusha), itafungwa 05/05/2013, Mwenge SDA Church.

-          Edger Emir Kapallah (Tegeta SDA) na Judith George Mabula (Mwanza), itafungwa 27/04/2013, Tegeta SDA Church.

-          Julius Jackson Nywage (Tegeta SDA) na Dina George Haule (Luhanga SDA-Iringa), itafungwa, 28/04/2013, Mwenge SDA Church.

17. Zamu:

-          mzee wa zamu: Eraga Mjuli

-          shemasi mkuu wa zamu: Rafiki Msuya

-          Mashemasi wa Zamu (Someni Ubaoni zamu zenu)

18. Utaratibu wa Sabato ya leo—Tarehe 20.04.2013
TUKIO
TEGETA
WATOTO
Mhubiri
MZEE S.I.M.KAPAYA
MAMA MAINGU
Mwenyekiti
MZEE DAMBA OMARA

Fungu Kuu na Ombi
MZEE ERAGA MJULI

Sadaka & zaka
MZEE R.BARIKESHA

Kufunga Sabato
MAMA RAHABU MORRO


19. Utaratibu wa Sabato ijayo—Tarehe 27.04.2013
TUKIO
TEGETA
WATOTO
Mhubiri
MZEE ERAGA MJULI
MAMA NYAIBAGO
Mwenyekiti
MWINJ. DICKSON JOSEPH MIPAWA

Ombi na Fungu Kuu
NDG. ALEX MAFURU

Sadaka/Zaka
NDG. ISAYA CHARLES

Maombi J5 (Asb.+Jioni)
MZEE S.I.M.KAPAYA

Kufungua Sabato
NDG. ELIYA KENANI

No comments

Powered by Blogger.