TEGETA SDA

TEGETA SDA

KARIBUNI KWENYE BLOGU YA KANISA LA TEGETA

Nawasalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, Karibuni katika blogu ya Kanisa la waadventista wasabato Tegeta, wakati unaenda mbio, maendeleo pia yanatokea kwa kasi, na sisi kama wasio wa ulimwengu huu lakini tukiwa ulimwenguni, twasafiri humu, hivyo tusimame imara katika imani. 
Pia tunamshukuru Mungu kwa ushindi mkuu katika juma la uamsho la uwakili,  ambapo mtu 1 aliokolewa na pia katika majuma mawili ya effort ambako watu 15 waliokolewa na kubatizwa katika maji mengi, kama lilivyo agizo lake Mungu. Mathayo 3:16.
Maendeleo katika technologia ya mawasiliano na habari yamekuwa ni chachu kubwa kwa Injili ya Yesu Kristo, nasi kama chombo cha Mungu Duniani, tumepewa ujumbe kuufikisha kwa watu wote kwa wakati, hivyo teknohama ni jukwaa ambalo twaweza kulitumia kwa kufanikisha utume wetu. (Math. 28:18-20).
  1. tegetasdachurch@blogspot.com
  2. twitter.com/tegetasdachurch
  3. facebook.com/tegeta.sdachurch
  4. tegeta.sdachurch@facebook.com
  5. tegetasdachurch@gmail.com
Wenu Shambani mwa BWANA, na Mtumwa wake Kristo,
Mwinjilisti: Saganga M. KAPAYA
Mzee wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tegeta (2013)



1 comment:

  1. Blog hii inatumika mpaka sasa?by masasi 2017 march 18

    ReplyDelete

Powered by Blogger.