TEGETA SDA

TEGETA SDA

MATANGAZO YA KANISA YA SABATO YA TAREHE 31/08/2013

MATANGAZO YA KANISA: 31/08/2013
1.       Tunamshukuru na kumtukuza Mungu wetu kwa neema na mibaraka yake, Wageni kwa wenyeji karibuni katika kanisa la Mungu na Ibada takatifu.

2.        (KUPITISHA WANATENDAKAZI) Tunapenda kuwapongeza wale waliokubali kumtumikia Mungu kwa nyadhifa mbalimbali kanisani.
3.       Effort yetu ya mtaa itaanza 5-19/10/013.Tafadhali tuendelea kutoa michango yetu ili kukamilisha na kufanikisha effort hiyo. Tutachangia 4,000,000/
4.        (TAARIFA: KIWANJA CHA KONDO), kiwanja chetu cha Kondo, kimevamiwa na Kanisa la Walokole. tunaendelea kufuatilia hati za kiwanja wizarani ili kupewa umiliki kamili. Tuliombee jambo hili kwa bidii. 1,200,000/=
5.       Tarehe 8/9/2013. Mtaa wetu wa Tegeta, tutakuwa na ugeni maalumu kutoka, G.C. (Mashauri kuu ya Kanisa),  Makamu mwenza wa mwenyekiti wa G.C. Mch. Geofrey Mbwana, atakuja kuweka jiwe la msingi la Nyumba la Mchungaji. Kanisa letu tunahitaji kuchangia 770,000/= kuchangia tukio hilo.
6.       Marekebisho ya choo, hali yake siyo nzuri, tunahitaji kuchangia 250,000/= kwa ajili ya marekebisho ya choo. Kuweka masinki ya kuflashi na mabomba.
Ø  Jumla ya fedha yote inayohitajika wiki hii ni; 1,200,000+770,000+250,000=2,220,000/
7.       Tuandae taarifa zote za robo ya 3 na  ziletwe kwa mchungaji mwisho Tarehe 15/09/13. Robo hii ya tatu
8.       Tutakuwa na baraza la kanisa, la dharura kesho saa 1:00 asubuhi. Tuhudhurie kwa wakati.
9.       Kutakuwa na kambi la Vijana (Masterguide Convention), Kampala, Bugema University. 4-8/12/20013.
a.       Gharama ni kiingilio $7 (kama TAS 11,327), malazi/chakula $7.5 (kama TAS 12,136) kwa siku, au malazi peke yake $3 (kama TAS 4,854), pia  usafiri mpaka kampala makanisa yatajitegemea. Kama utashiriki matukio yote mawili kiingilio ni $12 badala ya $14. Kanisa tushirikiane kuwawezesha vijana
10.    Kutakuwa na kongamano la muziki, Kampala, Bugema University. 9-15/12/20013,
a.       Gharama ni kiingilio $7 (kama TAS 11,327) kwa siku, au malazi peke yake $3 (kama TAS 4,854), pia  usafiri mpaka kampala makanisa yatajitegemea. Kama utashiriki matukio yote mawili kiingilio ni $12 badala ya $14.,  
b.       Ndg. Isaac Webi ameteuliwa kuratibu mpango huo kwa kanisa letu. Muoneni kwa maelezo zaidi. waimbaji na viongozi wa muziki kanisani, jiandaeni kwa kuhudhuria, Kanisa tushirikiane kuwawezesha wanamuziki wa kanisa.
c.        Kwa maelezo zaidi kuhusu matukio haya tembeleeni, wavuti ya divisheni: http://www.ecd.adventist.org
11.    Tarehe leo ni sabato ya idara ya wana wa kike: msisitizo wa kuzuia unyanyasaji, SASABASI! (END IT NOW!). Mchana tutakuwa na somo hilo maalumu, na pia taarifa ya waliokwenda Kigali. Karibuni nyote
12.    Wagonjwa:
a.       Mama Daktari Andrew, anaumwa, yuko nyumbani,
b.       Bi Upendo Maingu anaumwa, yuko nyumani,
c.        Mzee Joseph Msuya anaumwa,
Ø  tuwatembelee na kumuombea ili kuwafariji
13.    Matoleo: ya sabato iliyopita ni:…………………………………….  
14.    Zamu: Mzee wa zamu;             Mzee Damba Omara. Shemasi Mkuu wa zamu, Mzee Elia Kenani.
15.    Ratiba Fupi ya Wahudumu:
HUDUMA HUSIKA
MHUDUMU (SABATO LEO, 24/08/2013)
MHUDUMU (SABATO IJAYO, 31/08/2013)
Mhubiri
(Watoto)
 Ndg. Isaya Charles
Bi. Rafiki Msuya
Mhubiri (Wakubwa)
Mch. John R.Nyaibago
Mzee Damba Omara
Mwenyekiti
Ndg.  Anania Mndeme
Mzee Elia Kenani
Fungu Kuu na Ombi
Ndg. Enock Nyange
Ndg. Anania Mndeme
Sadaka & zaka
Ndg. Amos Obadia
Ndg. Isaya Charles
Kufunga Sabato
Ndg. Anania Mndeme

Jumatano (Asb)
Mzee Damba Omara

Jumatano (Jioni)
Ndg. Anania Masasi

Kufungua Sabato
Mwj. Editha Sanga


Ahsanteni, Mungu Awabariki!


MAELEKEZO YA MCHUNGAJI TANGAZO NA 5:

SEPT 8,2013 Itakuwa siku maalum katika mtaa wetu wa Tegeta.Ni siku ya kuweka jiwe la msingi na kuleta michango yetu ya kumalizia ujenzi wa Nyumba ya mchungaji.Siku hiyo itaongozwa na Kiongozi wetu wa kanisa katika ngazi ya Ulimwengu mch.Geofrey Mbwana ambaye ni makamu wa Mwenyekiti wa GC.

Pamoja naye watakuwepo wageni toka Tanzania Union na Toka Conf.yetu ya ETC.Wageni wengine tunaowategemea ni wachungaji na Wazee au wakilishi  toka katika mitaa ya Dar.

Pia Kwaya ya Mbiu pamoja na Pf toka kanisa la Kimanga watakaoendesha Gwaride maalum la kukaribisha wageni. Kutakuwepo pia wageni mbalimbali walioalikwa kwa ajili ya siku hiyo.

Kwa sababu ya umuhimu wa siku hiyo, Tunawaomba vijana wetu wakiongozwa na kamanda wetu wa mtaa ndg  Nehemia Ibrahamu kuandaa progrm maalum ya kukaribisha wageni; Kwaya zetu zote za makanisa toka mtaani wajiendee kushirikiana na kwaya ngeni katika   programu maaalum ya uimbaji  chini ya kiongozi wa kwaya mtaa ndg Isaac Webi katika siku hiyo Itapendeza mkiwa katika unifomu.

Program zetu zitaanza saa 2.00- saa 8.00 mchana. Tunatiwa moyo kubeba kipoza njaa ili kufanya utulivu katika siku hiyo. Hebu tutiane moyo washiriki wote wa mtaa wa Tegeta wadogo kwa wakubwa kuhudhuria Sherehe hii kubwa ya Kiroho.

Hii imekuja kuimarisha umoja wetu pia. Kumbuka ni kile ambacho kwa neema ya Bwana tumekifanya cha Kuasisi ujenzi wa Nyumba ya mch.na tumekuwa wa kwanza kuitikia jambo hili la muhimu katika Conf. Yetu na wameamua kualika mitaa mingine kuja kujifunza kwetu. Hebu sasa tuje kwa kishindo kumalizia kazi hii. Ukiweza kuaalika hata marafiki wasio Waadventista njoo nao itakuwa ni ibada ya pekee siku hiyo.


 Kamati mbali mbali za maandalizi ya tukio hili kubwa tafadhali tuwajibike kama tulivyokubaliana katika baraza la mtaa ili kufanikisha maandalizi.Tunatiwa moyo ili kutoa michango yetu kidogo ili kukaribisha wageni wa siku hiyo.Kumbuka dalili moja ya mji ulio na baraka ni kutembelewa na wageni.N a neno la Mungu linatukumbusha kuwa  “Msisahau kuwafadhili wageni; maana kwa njia hii wengine wamewakaribisha malaika pasipo kujua.” Webr 13:2

No comments

Powered by Blogger.