TEGETA SDA

TEGETA SDA

MATANGAZO YA KANISA YA SABATO YA TAREHE 24/08/2013

MATANGAZO YA KANISA: 24/08/2013
1.       Tunamshukuru na kumtukuza Mungu wetu kwa neema na mibaraka yake, tunamshukuru kwa kutupa makambi mwaka huu. Wageni kwa wenyeji karibuni katika kanisa la Mungu na Ibada takatifu.

2.       (KUWAPOKEA WABATIZWA) Tunamtukuza Mungu kwa kanisa kupata washiriki wapya waliompokea Yesu na kubatizwa (idad 3)
3.       (KUPITISHA WANAKWAYA) Tunapenda kuwapongeza wale walioamua kumtumikia Mungu kwa njia ya uimbaji. Tunawakaribisha wengine pia.
4.       (TAARIFA: KIWANJA CHA KONDO), kiwanja chetu cha Kondo, kimevamiwa na Kanisa la Walokole. tunaendelea kufuatilia hati za kiwanja wizarani ili kupewa umiliki kamili. Tuliombee jambo hili kwa bidii.
5.       Effort yetu ya mtaa itaanza 5-19/10/013.Tafadhali tuendelea kutoa michango yetu ili kukamilisha na kufanikisha effort hiyo. Goli la kanisa letu ni 4,000,000/
6.       Tuandae taarifa zote za robo ya 3 na  ziletwe kwa mchungaji mwisho Tarehe 15/09/13. Robo hii ya tatu
7.       Kamati za makambi, yaliyomalizika andaeni taarifa kwa ajili kuzileta katika katika kikao cha mtaa. Kikao cha mtaa cha kawaida kwa robo kitafanyika, kesho 24/08/2013  katika kanisa la Tegeta.
8.       Leo, mchana saa 8:00, tutakuwa na washa (semina), ya neno la Mungu, Unabii. Tujiandae kwa ajili ya kujifunza, wabatizwa wapya muhudhurie bila kukosa.
9.       Tutakuwa na baraza la kanisa, la dharura leo jioni, saa 10:00 Tuhudhurie kwa wakati.
10.    Kutakuwa na kambi la Vijana (Masterguide Convention), Kampala, Bugema University. 4-8/12/20013.
a.       Gharama ni kiingilio $7 (kama TAS 11,327), malazi/chakula $7.5 (kama TAS 12,136) kwa siku, au malazi peke yake $3 (kama TAS 4,854), pia  usafiri mpaka kampala makanisa yatajitegemea. Kama utashiriki matukio yote mawili kiingilio ni $12 badala ya $14. Kanisa tushirikiane kuwawezesha vijana
11.    Kutakuwa na kongamano la muziki, Kampala, Bugema University. 9-15/12/20013,
a.       Gharama ni kiingilio $7 (kama TAS 11,327) kwa siku, au malazi peke yake $3 (kama TAS 4,854), pia  usafiri mpaka kampala makanisa yatajitegemea. Kama utashiriki matukio yote mawili kiingilio ni $12 badala ya $14.,  
b.       Ndg. Isaac Webi ameteuliwa kuratibu mpango huo kwa kanisa letu. Muoneni kwa maelezo zaidi. waimbaji na viongozi wa muziki kanisani, jiandaeni kwa kuhudhuria, Kanisa tushirikiane kuwawezesha wanamuziki wa kanisa.
c.        Kwa maelezo zaidi kuhusu matukio haya tembeleeni, wavuti ya divisheni: http://www.ecd.adventist.org
12.    Tarehe 3/9/2013 ni sabato ya idara ya wana wa kike: msisitizo wa kuzuia unyanyasaji, SASABASI! (END IT NOW!). Somo limewasili, idara ya wana wa kike tunawaomba mjiandae, sabato ijayo tutakuwa na somo hilo maalumu.
13.    Wagonjwa: Mama Daktari Andrew, amefanyiwa upasuaji, hospitali ya Lugalo, tumuombee na kumtembelea ili kumfariji.
Bi Joyce /Malima Martin, anaumwa, washiriki tunombwa tumtembelee kwake, Nyaishozi (chasimba?) na kumfariji.
14.    Matoleo: ya sabato iliyopita ni:…………………………………….
    
15.    Zamu: Mzee wa zamu;             Mzee Saganga  Kapaya. Shemasi Mkuu wa zamu, Mzee Elia Kenani.
16.    Ratiba Fupi ya Wahudumu:
HUDUMA HUSIKA
MHUDUMU (SABATO LEO, 24/08/2013)
MHUDUMU (SABATO IJAYO, 31/08/2013)
Mhubiri
(Watoto)
Bi. Upendo Maingu
Mzee Joseph Msuya
Mhubiri (Wakubwa)
Ndg. Daudi Kubhoja
Ndg. Fred Maiga
Mwenyekiti
Mzee B.I.Morro
Ndg.  Anania Mndeme
Fungu Kuu na Ombi
Mzee Damba Omara
Ndg. Enock Nyange
Sadaka & zaka
Ndg. Anania Masasi
Ndg. Amos Obadia
Kufunga Sabato
Mzee John Kamuli
Ndg. Anania Mndeme
Jumatano (Asb)
Mzee Zihirwani Chikira

Jumatano (Jioni)
Ndg. Anania Masasi

Kufungua Sabato
Ndg. Daudi Kubhoja



Ahsanteni, Mungu Awabariki!

No comments

Powered by Blogger.